Nenda kwa yaliyomo

Umoja wa Ulaya

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
(Elekezwa kutoka European Union)
Umoja wa Ulaya
European Union (EU)
Kaulimbiu: "United in diversity" ("Umoja katika utofauti")
Wimbo wa taifa: "Ode to Joy"
Mahali pa Umoja wa Ulaya
Mji mkuuBrussels (de facto)
Mji mkubwaBerlin
Bahari ya Atlantiki, Bahari ya Mediterania, Bahari ya Kaskazini, Bahari ya Baltic
Lugha rasmiKiholanzi, Kiingereza, Kifaransa, Kijerumani, Kihispania, Kiitaliano, na lugha nyingine 18
Lugha ya taifaLugha za mataifa wanachama
 • Rais wa Baraza la Ulaya
Charles Michel
 • Rais wa Tume ya Ulaya
Ursula von der Leyen
Muungano
 • Mkataba wa Maastricht
1993
 • Kuanzishwa kwa Euro
1999
 • Brexit (Uingereza kujiondoa)
2020
Eneo
 • Jumlakm2 4,233,255 (ya 7)
 • Maji (asilimia)3%
Idadi ya watu
 • Kadirio la 2025 448,400,000
PLT (PPP)Kadirio la 2025
 • Jumla $29.005 trilioni
 • Kwa kila mtu $64,080
PLT (Kawaida)Kadirio la 2025
 • Jumla $20.287 trilioni
 • Kwa kila mtu $43,194
HDI (2021) 0.899 (HDI)
Gini (2022)29.6
SarafuEuro
Majira ya saaUTC+1 CET / CEST (UTC+2)
Upande wa magariKushoto na kulia (inategemea nchi)
Msimbo wa simu++3 , +4
Tovuti rasmi:
https://europa.eu
Tanbihi:
Data inatokana na Jumla au wastani wa data ya mataifa ya Umoja wa Ulaya

Umoja wa Ulaya (kifupisho: EU) ni muungano wa kisiasa na wa kiuchumi wa nchi 27 za Ulaya, baada ya Ufalme wa Muungano kujitoa tarehe 31 Januari 2020, tukio la kwanza la namna hiyo. Ulianzishwa mwaka 1991 juu ya msingi wa Jumuiya ya Kiuchumi ya Ulaya.

Shabaha kuu zilikuwa kujenga uchumi wa pamoja, kuboresha maisha ya watu wa Ulaya na kuzuia vita kati ya nchi za Ulaya.

Nchi 19 za Umoja huo hutumia pesa moja ya Euro.

Nchi nyingi za Umoja zimepatana kufungua mipaka yao bila vizuizi kwa wakazi wote.

European Commission (Brussels)

Historia

[hariri | hariri chanzo]

Jumuiya ya Kiuchumi ya Ulaya ilibadilisha jina lake mwaka 1992 kufuatana na mikataba ya Maastricht kuwa Umoja wa Ulaya.

Nchi wanachama zilipatana kujenga siasa ya pamoja ya kiuchumi, kifedha, kisheria na katika mambo ya nje.

Mapatano ya Schengen ilifungua mipaka ili wakazi wa nchi hizo waweze kusafiri bila pasipoti wala vibali.

Nchi 10 tena zilijiunga na Umoja wa Ulaya mwaka 2004. Mbili zaidi ziliingia 2007 na Kroatia mwaka 2013.

Demografia

[hariri | hariri chanzo]

Jumla ya wakazi ni milioni 447 (mwanzoni mwa 2020), sawa na 5.8% za watu wote duniani. Kuna miji 15 yenye watu zaidi ya milioni moja kila mmojawapo, kuanzia Paris ambayo inazidi milioni 10.

Upande wa lugha, lugha rasmi ni 24, lakini lugha inayotumika zaidi ni Kiingereza, kinachoweza kuzungumzwa na 51% za wakazi wote, ingawa ni lugha ya kwanza ya 1% tu. Lugha nyingine ambazo ni za kwanza kwa wananchi wengi ni: Kijerumani (18%), Kifaransa (13%) na Kiitalia (12%). Pia kuna lugha 150 hivi za kieneo.

Upande wa dini, wakazi wengi ni Wakristo (71.6%), hasa Wakatoliki (45.3%), Waprotestanti 11.1% na Waorthodoksi 9.6%. Waislamu ni 1.8%. Wafuasi wa dini nyingine ni 2.6%. Wengine 24% hawana dini au ni Wakanamungu.

Uhuru wa kuhama

[hariri | hariri chanzo]

Kila mtu mwenye uraia wa nchi ya Umoja anaruhusiwa kuhamia nchi yoyote nyingine na kufanya kazi au biashara huko bila vibali vya pekee.

Vilevile bidhaa zote zinazotengenezwa kote katika Umoja wa Ulaya zinaweza kuuzwa katika kila nchi. Hii ni sababu ya kuwa na sheria za pamoja zinazotawala masharti ya bidhaa na uzalishaji.

Utawala na Serikali

[hariri | hariri chanzo]

Halmashauri ya Ulaya

[hariri | hariri chanzo]

Halmashauri hii ni mkutano wa viongozi wa serikali za nchi wanachama. Wanakutana mara mbili kwa mwaka na kutoa maazimo muhimu.

Nafasi ya uraisi hubadilika kila baada ya miezi 6. Ufini ilishika uraisi kati ya Julai 2006 hadi Desemba 2006, ikafuatiliwa na Ujerumani tangu Januari hadi Juni 2007.

Baraza za mawaziri

[hariri | hariri chanzo]

Katika baraza hizi mawaziri ya Kilimo, Sheria, Mambo ya Nje hukutana na kupanga siasa ya pamoja.

Kamati ya Ulaya

[hariri | hariri chanzo]

Hii ni kamati ya utawala inayotekeleza maazimio ya Halmashauri na bunge. Kuna makamishna 24 na mwenyekiti. Inaelekea kuwa serikali lakini haina madaraka ya serikali bado.

Bunge la Ulaya

[hariri | hariri chanzo]
Bunge la Umojwa wa Ulaya huko Brussels.
Picha ya pamoja wakati wa kusaini mkataba wa Lisboa tarehe 13 Desemba 2007.

Bunge la Ulaya lina wabunge 751 wanaochaguliwa na wananchi kila baada ya miaka mitano.

Wanachama

[hariri | hariri chanzo]
CroatiaFinlandSwedenEstoniaLatviaLithuaniaPolandiSlovakiaHungaryRomaniaBulgariaGreeceCyprusCzech RepublicAustriaSloveniaItalyMaltaPortugalSpainFranceGermanyLuxembourgBelgiumNetherlandsDenmarkIreland
Map showing the member states of the European Union (clickable)

Wanachama tangu 1958 (waanzilishi)

[hariri | hariri chanzo]

Wanachama tangu 1973

[hariri | hariri chanzo]

Mwanachama tangu 1981

[hariri | hariri chanzo]

Wanachama tangu 1986

[hariri | hariri chanzo]

Wanachama tangu 1995

[hariri | hariri chanzo]

Wanachama tangu 2004

[hariri | hariri chanzo]

Wanachama tangu 2007

[hariri | hariri chanzo]

Wanachama tangu 2013

[hariri | hariri chanzo]

Nchi zinazoomba uanachama

[hariri | hariri chanzo]

Jeshi la Uropa/Ulaya

[hariri | hariri chanzo]

Tazama pia

[hariri | hariri chanzo]

Viungo vya nje

[hariri | hariri chanzo]

Tovuti rasmi:

Mandhari na data:

Taarifa:

Misaada ya kufundishia:

Viungo vya nje

[hariri | hariri chanzo]
WikiMedia Commons
WikiMedia Commons
Makala hii kuhusu maeneo ya Ulaya bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Umoja wa Ulaya kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.