Kingala (Kongo)
Kilingala (au Lingala) ni lugha ya Kibantu hasa nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo ambako ni lugha ya taifa na Jamhuri ya Kongo ambako pia imetambulika rasmi. Tena kuna wasemaji wa Kingala nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati, Angola n.k. Kufuatana na uainishaji wa lugha za Kibantu wa Malcolm Guthrie Kilingala kiko katika kundi la C40.
Kinazungumzwa hasa na Wangala.
Mwaka wa 2024 idadi ya wasemaji wa Kilingala kama lugha ya kwanza imehesabiwa kuwa watu milioni 20; pamoja na hayo kuna watu milioni 20 tena ambao huongea Kilingala kama lugha ya pili.
Mfano wa kuandikwa kwa Kingala
[hariri | hariri chanzo]Bato nyonso na mbotama bazali nzomi pe bakokani na limemya pe makoki. Bazali na mayele pe base, geli kofanda na bondeko okati na bango.
Tafsiri katika Kiswahili
[hariri | hariri chanzo]Watu wote wamezaliwa huru, hadhi na haki zao ni sawa. Wote wamejaliwa akili na dhamiri, hivyo yapasa watendeane kindugu.
Viungo vya nje
[hariri | hariri chanzo]- lugha ya Kilingala kwenye Multitree
- makala za OLAC kuhusu Kilingala Ilihifadhiwa 24 Juni 2013 kwenye Wayback Machine.
- lugha ya Kilingala katika Glottolog
- http://www.ethnologue.com/language/lin
![]() |
Makala hii kuhusu mambo ya lugha bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Kingala (Kongo) kama historia yake, uenezi au maendeleo yake? Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |