Nenda kwa yaliyomo

Uskoti

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
(Elekezwa kutoka Scotland)
Uskoti
Scotland (Kiskoti)
Alba (Kigaeli)
Wimbo wa taifa: "Flower of Scotland" (hutumika zaidi)
Eneo la Uskoti katika Ufalme wa Muungano
Mji mkuu
na mkubwa
Edinburgh
Lugha rasmi
  • Kiingereza
  • Kiskoti
  • Kigaeli cha Uskoti
  • Lugha ya Ishara ya Uingereza
Kabila
Dini
 • Mfalme
Charles III
 • Waziri Mkuu wa Uskoti
John Swinney
Eneo
 • Jumlakm2 80,231
Idadi ya watu
 • Kadirio la 20225,439,842
 • Msongamano70/km2
PLT (Kawaida)Kadirio la
 • Jumla£218.0 bilioni
 • Kwa kila mtu£39,707
HDI (2022)0.933 juu sana
SarafuPauni ya Uingereza (GBP)
Majira ya saaUTCUTC+0 (GMT)
Upande wa magariKulia
Msimbo wa simu++44
Jina la kikoa.scot

Uskoti, (kwa Kiingereza:Scotland , Alba kwa Kigaeli) , ni nchi ndani ya Ufalme wa Muungano, iliyoko katika Ulaya ya Kaskazini. Inapakana na Uingereza kusini, na imezungukwa na Bahari ya Kaskazini mashariki, Bahari ya Atlantiki kaskazini na magharibi, na Bahari ya Ayalandi kusini-magharibi. Uskoti ina idadi ya watu takriban milioni 5.4, ikiwa ya 120 duniani. Mji wake mkuu ni Edinburgh, huku jiji kubwa zaidi likiwa Glasgow. Uskoti imegawanyika katika maeneo 32 ya halmashauri. Inajulikana kwa urithi wake tajiri wa Kikelti na Kigaeli, majumba ya kifalme ya kihistoria, maeneo ya milimani (Highlands), na mchango wake mkubwa katika falsafa, sayansi, na uhandisi wakati wa Enzi ya Mwangaza.

Jiografia

[hariri | hariri chanzo]

Uskoti ni theluthi ya kaskazini ya kisiwa cha Britania. Eneo lake ni km² 78,772. Upande wa kusini Uskoti umepakana na Uingereza wenyewe.

Upande wa mashariki kuna Bahari ya Kaskazini, upande wa kaskazini na magharibi ile ya Atlantiki pamoja na bahari ya Eire.

Ndani ya nchi kuna kanda tatu:

Mlima mkubwa wa Uskoti ni Mlima Nevis karibu na Fort William wenye kimo cha mita 1,344.

Mbali ya bara Uskoti ina visiwa 790. Upande wa magharibi wa Uskoti bara liko funguvisiwa la Hebridi. Upande wa kaskazini kuna visiwa vya Orkney na vya Shetland.

Historia

[hariri | hariri chanzo]

Kihistoria Uskoti uliwahi kuwa nchi ya pekee, mpaka ikaunganishwa chini ya Ufalme wa Uingereza tangu mwaka 1603 BK.

Tangu mwaka 1707 Uskoti haukuwa tena na bunge la pekee lakini ulikuwa na wawakilishi katika bunge la London. Bunge la Uskoti lilirudishwa tena mwaka 1999 nalo linasimamia mambo ya ndani.

Mnamo Septemba 2014, wananchi walipiga kura kuhusu uhuru wa nchi yao, lakini wengi waliamua kudumisha Ufalme wa Muungano. Hata hivyo, baada ya Ufalme huo kujitoa katika Umoja wa Ulaya, kuna mpango wa kupiga tena kura mwaka 2023.

Miji kumi mikubwa ya Uskoti

[hariri | hariri chanzo]
Mji Wakazi
5 Aprili 1991
Wakazi
29 Aprili 2001
Glasgow (Glaschu) 658.379 629.501
Edinburgh (Dùn Èideann) 400.632 430.082
Aberdeen (Obar Dhèathain) 182.133 184.788
Dundee (Dùn Dè, Dùn Dèagh) 157.808 154.674
Paisley (Paislig) 73.925 74.170
East Kilbride (Cille Bhrìghde an Ear) 70.579 73.796
Hamilton (Hamaltan) 49.988 48.546
Cumbernauld (Comainn nan Allt) 49.507 49.664
Greenock (Grianaig) 49.267 45.467
Ayr (Àir) 47.962 46.431

Picha za Uskoti

[hariri | hariri chanzo]

Viungo vya Nje

[hariri | hariri chanzo]
Makala hii kuhusu maeneo ya Ulaya bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Uskoti kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.